Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Tuesday, February 21, 2012

BIFU YA MR. TWO NA CLOUDS FM - TZ YAFIKA KIKOMO



MR.  TWO NA MKURUGENZI WA CLOUDS FM WAPATANISHWA.

Hatimaye ugomvi wa Mkurugenzi wa Clouds Media (cloudsfmTz) Ruge Mutahaba na Mbunge wa jimbo la Mbeya kwa tiketi ya CHADEMA  Joseph Mbilinyi (Mr. Two Sugu) umemalizika baada ya kufanyika kwa vikao mbali mbali chini ya Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo wa Tanzania.
  

RUGE


Hatua hii yatia kikomo ugomvi wa maneno makali na bifu katika muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania uliopelekea kutochezwa kwa nyimbo za kundi la Vinega na kutolewa kwa album mbili za kuwapaka matope wafanyikazi mbali mbali wa Clouds Radio na Tv.

Baadhi ya wasanii wa Mombasani walikuwa wamejaribu kuiga bifu hii. Swali ni je kwa sasa watachukua hatua gani?

Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

No comments:

Post a Comment