Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Wednesday, February 22, 2012

MSANII ANAPO'HIT NANI WA KUPEWA SHUKRANI?



NANI ANAYEFAA KUPEWA SHUKRANI BAADA YA MSANII KU’HIT KATIKA INDUSTRY?

Msanii hupitia safari ndefu, akipitia mikononi mwa washikadau mbali mbali katika sekta ya sanaa kabla ya ku’hit. Hata hivyo baada ya msanii kuafikia ndoto yake ya kupata umaarufu na mafanikio ya kifedha katika ulimwengu wa mziki, nani anafaa kupewa shukrani kufuatia mchango wake mkubwa ama umuhimu mkubwa katika kufanikisha haya yote?

Wengi tuna majibu tofauti kufuatia mitazamo yetu tofauti lakini ningeomba mwanzo huyu msanii mwenyewe tumtoe katika orodha ya majibu yetu kwa sababu ni yeye tunamzungumzia kwa leo.
Pili mwenyezi mungu ambaye sote tunakubaliana kwamba ni mwezesha wa yote katika sanaa, mwanzo wa kila kitu na ambaye hatupingi uwezo wake.

Sekta ya sanaa hususan hapa Mombasani imetajwa kushirikisha washikadau mbalimbali ikiwemo ma’producer,ma’promoter,ma’presenter na wasikilizaji.  Washikadau hawa hutekeleza majukumu mbali mbali na kuchangia kwa usawa katika kukua kwa sanaa ya mziki. Hata hivyo wengi ya wasanii niliokumbana nao katika harakati za kusukumu gurudumu la sanaa wameniuliza swali hili, “je tutakapo hit nani tumshukuru zaidi?” Katika uchanganuzi wa washikadau katika jamii kupitia mchango wa waskilizaji tukufu wa kipindi cha “Chipkizi Za Kaya”, tunapata picha kamili ya majukumu mbali mbali ya washkadau wakuu katika sekta ya mziki wa Mombasani.

Producer hua mwanzo wa safari nzima ya msanii na huchangia pakubwa katika kuasisi mafanikio ya msanii yeyote. Wengi ya ma’producer wetu huwa wajuzi wa sanaa ya mziki mbali nakufahamu vyema jinsi ya kuruka viunzi tofauti tofauti katika mbio za kutafuta mafanikio ya kimziki. Katika kipindi cha “Chipkizi Za Kaya” ndani ya Radio Kaya jumapili ya tarehe 19, baadhi ya wasikilizaji waliotoa michango yao kuhusiana na mjadala huu walimtaja producer kama kiungo muhimu zaidi. Wengi walidai yeye ndio hupika chakula ambacho wao hutokea kukipenda. Wakimlenganisha na mpishi jikoni, wengi wahoji kuwa producer nyakati zozote hushikilia funguo ya ufanisi kwa msanii kwani yeye ndio ataamua kuongeza ama kupunguza chumvi katika chakula ambacho msikilizaji ataamua kama nikitamu ama hakifai.

Promoter pia atajwa katika orodha ya washikadau wakuu katika sekta ya mziki ambao pia huchangia pakubwa katika ufanisi wa msanii hususan limbukeni ama anayechipuka. Promoter anasemekana kuwa mfadhili wa ndoto nzima ya msanii. Kulingana mashabiki waliotoa mchango wao, promoter pia anaeza kulinganishwa na mjasiriamali kwani katika mchakato mzima wa kumfadhili msanii, hua analenga kufaidika baada ya msanii kufanikiwa kupitia pesa zitakazo kusanywa wakati wa ma’show. Kufuatia kutotaka kupoteza mtaji alioekeza katika msanii, promoter hufanya kila awezalo kuhakikisha msanii ana’hit katika industry. Pia wengi  washikilia kuwa promoter  hua katika stage muhimu ya usanii. Stage ya uasisi wa ndoto nzima. Bila yeye msanii huvunjika moyo na  wengine huachana na maswala ya mziki huku uwepo wa support yake humtia moyo msanii kufanya bidii. Katika pointi hii msikilizaji mmoja amfananisha promoter na mzazi kwa mwanafunzi, ambapo humlipia fees na kumuachia mwanafunzi jukumu la kutia bidii kufanikiwa.

Presenter tunazungumzia mtangazaji wa redio ambaye hucheza wimbo wa msanii na kumtambulisha kwa mshikadau mwengine ambaye ni msikilizaji. Wengi walisistiza ulazima katika kuwepo kwa uhusiano mwema kati ya mshikadau huyu na yule awali kwa jina promoter. Wasikilizaji wengi wadai uhusiano huu hua na mchango mkubwa katika jinsi msanii atakavyowasilishwa kwa maskio ya waskilizaji. Kazi ya presenter kitaaluma huhusisha kuskiliza kazi za msanii na kuamua iwapo zitawaburudisha wasikilizaji wake anapokua hewani. Jukumu hili alitwekwa baada ya kubainika kwamba kufuatia uzoefu wake katika kazi, anaweza kujua ni aina gani ya mziki msikilizaji wake hupenda. Baadhi ya waskilizaji waliochangia mjadala huu pia walihoji kuwa presenter hua na mamlaka ya kuamua kucheza ama kutocheza nyimbo. Jambo hili latajwa kumgeuza na kuwa wa muhimu zaidi katika mafanikio ya msanii. Swala la mshikadau huyu kuwa na uwezo wa kucheza ama kutocheza nyimbo hata anapoombwa na msikilizaji hewani latajwa kumpa uzito zaidi katika ratili ya mchakato huu.

Msikilizaji  ni yule anayeshabikia msanii katika redio. Mara nyingi hushirikiana kwa sana na presenter katika vipindi kabla ya kujiunga na mapromoter na msanii mwenyewe katika sehemu za burudani. Mara nyingi hupiga simu kuomba wimbo ama kuketi chini na kuskiza mziki unaochezwa katika kipindi. Kulingana na wengi waliochangia katika “Chipkizi Za Kaya” mshikadau huyu ni miongoni mwa wale wakuu katika game, kwani yeye ndiye anayetengenezewa nyimbo. Msanii anapo amua usanii lengo lake kubwa huwa ni kumrai na kumfurahisha msikilizaji. Promoter anapoamua kumfadhili msanii hulenga kufaidika baadaye msikilizaji huyu anapojitokeza katika sehemu za burudani kumwona msanii mwenyewe.

Presenter humtegemea sana mshikadau huyu kimaisha kwani yote anayofanya katika kazi yake hua ni kuhakikisha msikilizaji anafurahi na kuganda katika kipindi chake kila uchao. Kwa vile msikilizaji anaamua mwenyewe nyimbo gani inayo mfurahisha, presenter mara nyingi hana budi bali kucheza wimbo ule msikilizaji anaoufagilia zaidi. Katika muktadha huu, wengi ya walioshiriki mjadala huu walikubaliana kwamba shabiki  huamua  ni nyimbo gani inayo hit. Mskilizaji pia atajwa kuwafanya ma’promoter, ma’ presenter na ma’ producer kuwa busy kwani wote huwa katika harakati za kujaribu kumridhisha mshikadau huyu. Umuhimu wake watajwa kuongezeka zaidi pale anapopewa nafasi na presenter kuchagua wimbo utakaochezwa katika vipindi vya redioni.

Je nani anayefaa kupewa shukrani baada ya msanii ku’hit katika industry?



 (c)mwanamgambo2012



No comments:

Post a Comment