Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Friday, February 17, 2012



“RUDI NYUMBANI MWANANGU”

Mama wa msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Ray C ambaye majina yake kamili ni Rehema Chalamila amtaka mwanaye kurudi kwao nchini Tanzania.

 Kwa mujibu wa ndugu wa karibu wa Ray C mamake Ray C hajafurahia kitendo cha mwanaye kuhamia jijini Nairobi na akamtaka kurudi  Bongo ili awe karibu naye.

Kulingana na nduguye Mamayake anataka Ray C arudi kuja kufanya shughuli zake za kimuziki Bongo kwani hufurahi kumuona mara kwa mara .

Mwanzoni mwa wiki hii mamake Ray C huyo alisikika akizungumza katika Kipindi cha stesheni mmoja nchini  Tanzania na alikiri kutamani kwake kumuona mwanawe amerudi nyumbani.

Mamake Ray C asema hakumpa Ray C baraka za kuja kuishi Kenya na akasistiza angependa mwanae arudi nchini Tanzania na kumuimbia mungu.

Kwa sasa Ray C anaishi nchini Kenya na kufanya shughuli zake za kimuziki nchini jijini Nairobi na hivi karibuni alizindua bendi  yake.

Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

No comments:

Post a Comment