Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Saturday, February 18, 2012

"DUDUBAYA APANGA KUHAMA DAR"



DUDUBAYA KUHAMA DAR ES SALAAM KARIBUNI.

MSANII wa Bongo Fleva, Godfrey Tumaini aka Dudubaya anaeishi area 88.4 Dar es salaam nchini Tanzania,  ametangaza rasmi kupitia mtandao mmoja wa kijamii kwamba anajipanga kuihama Dar es Salaam na kwenda kuishi kwao Kiseza huko Mwanza  katika kipindi cha miaka mitatu ijayo.

Dudubaya asema sababu mbili kubwa zinazomfanya kuuhama mji mkuu wa Tanzania Dar es Salaam na kuelekea mkoa wa Mwanza ni  joto na jam za barabarani, ambazo amedai humchelewesha kila mara .

Dudubaya ambae alianza maisha ya kujitegemea jijini Dar es salaam miaka saba iliyopita, amesema kwa sasa anakaribia kumalizia nyumba yake anayoijenga  nyumbani kwao Mwanza, ambayo anadai imemgharimu shilingi milioni kumi pesa za Tanzania.

Kwa sasa Dudubaya anamiliki  kampuni moja inayojihusisha na kuuza madirisha na milango ya mbao, pamoja na kampuni ya kuandaa show za wasanii kwenye mikoa mbalimbali ya Tanzania hukuakijihusisha na ulimwengu wa filamu za kibongo pia.


Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

No comments:

Post a Comment