Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Sunday, February 19, 2012

LAI AACHILIA WIMBO MPYA – “USIKONDE”




MSANII  LAI  AACHILIA  NYIMBO MPYA KWA JINA  – “USIKONDE”

Msanii wa mziki wa Mombasani Ngala Lai Mwangala maarufu Lai ameachlia ngoma yake mpya kwa jina “Uskonde”.

Lai ambaye pia ni “Producer” wa studio za Crack SoundsMariakani, alizaliwa sehemu ya Mtaani mjini Kilifi katika kaunti ya Kilifi.

Ni mzaliwa wa tatu katika familia ya watoto wanne na ndugu wa tumbo moja na “producer” mwegine mkali Mombasani  producerJay Crack Mfalme wa Crack Sounds - Kilifi.

Alisoma katika shule ya msingi ya Kilifi Primary School kabla ya kujiunga na shule ya upili ya St. Anthony –  Karatina.

Akizungumza na “kaya FlavazLai afichua kuwa alianza mziki “seriously” mwaka wa 2007 kabla ya kupata nafasi ya kurekodi wimbo wake wa kwanza mwaka mmoja baadaye – 2008.Lai asema alirekodi waimbo wake wa kwanza katika studio za FP Records mwaka wa 2008, nyakati hizo studio hiyo inapatikana Watamu.

Wimbo wake wa kwanza ulikuwa unaitwa “Madem” na alikua ameshirikisha wasanii wakali wa nyakati hizo “Majizee

Katika mipango yake ya baadaye Lai afichuaa kuwa anajipanga kumaliza kusomea taaluma ya “Visual and Sound Engineering” katika chuo cha “Home Boys” jijini Nairobi.

Akifunguka kuhusu maisha yake ya kibinafsi Lai asema anam’date mrembo mmoja ambaye wakereketwa wa sanaa ya Mombasani wanamjua kama Mummy D, ambaye pia ni msanii.

Asipokuwa mitambano, Lai asema yeye hupenda kuhudhuria masomo ya bibilia na kufichua kuwa kila jumapili hushiriki maombi katika kanisa la Royal Tarbanacle na pastor wake ni Shadrack Ndune.

Akizungumzia “game” ya Mombasani, Lai ataja ukosefu wa “seriousness” miongoni mwa  wasanii wa mombasani kama sababu kuu ya sanaa kutopiga hatua za kimaendeleo licha ya uwepo wa wasanii wenye vipaji.

“Watu wengine waingia “game”na hawajajipanga ama hawako “serious”. Mtu ataingiaje “game” na 4000/= pesa  za kurekodi! Nairobi msanii chipkizi anaingia game na “manager” na “budget” kubwa ya hela kufadhili mwanzo wa “career” yake. Ni kama anafanya "investment" ya biashara. Huku kwetu watu wanafanya mziki kama “fun”…….ndio maana mziki ama sanaa ya Mombasa nayo inawachukulia”fun” pia”, akamalizia.

Akizungumza kuhusu wimbo ake mpya Lai asema wimbo huu unalenga kila mmoja katika jamii na unawapa moyo wanajamii licha ya hali ngumu za kimaisha.

Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.


LAI - USIKONDE


Contacts:
http://www.facebook/Lai Mwangala
laimwangala@yahoo.com

No comments:

Post a Comment