Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Sunday, February 19, 2012

MR.BADO ADONDOSHA PINI JIPYA - "MACHOZI"



MR.BADO ADONDOSHEA MASHABIKI WAKE NYIMBO MPYA - "MACHOZI." AKIMSHIRIKISHA DADAKE

Mr. Bado a.k.a Mzungugiryama

Ni Msanii aliyezaliwa huko  Malindi sehemu ya Watamu katika kaunti ya Kilifi. Alizaliwa mnamo tarehe 15 Desemba mwaka wa 1980. Ni mwana wa msanii Maarufu wa ngoma za kitamaduni za jamii ya Wamijikenda; Mzee Nyerere Wa Konde na Mama Mariam Mohammmed. Ni mtoto wa tano katika familia hii iliyojaliwa watato 10.

Mr. Bado a.k.a Mzungugiryama ambaye majina yake halisi ni Mohammed Said Ngana, alipata masomo yake ya msingi katika shule ya msingi ya Gede Primary School kabla ya kujiunga na shule ya upili ya Barani Secondary School mjini Malindi.

Mr. Bado afichua kuwa usanii wake ulianza kitambo na babake Mzee Nyerere Wa Konde alichangia pakubwa katika yeye kupenda maswala ya mziki na utumbuizaji. Mr. Bado anakumbuka kwa madaha kisa ambacho kilichootesha ari yake ya kuwa mwanamziki. Mr. Bado anasema aliwahi kutumbuiza umati mkubwa akiwa na umri mdogo, ambapo ilikuwa ni mwaka wa 1990 wakati wa matanga ya marehemu nyanyake. Babake ambaye alikua anatumbuiza umati kwa nyimbo zake za kimijikenda alimshika mkono na kumvuta mbele ya umati akimtaka amsaidie katika kutumbuiza watu.

Hata hivyo alianza maswala ya mziki hususan wa kizazi kipya “seriously” mwaka wa 1996 na toka mwaka huo hadi sasa anasema ari yake ya kutaka kufanikiwa kimziki haijawahi kufifia. 

Wimbo wake wakwanza uliomtambulisha kwa mashabiki wa “ngomapwani” anasema ni “Stand By Me “ aliourekodi mwaka wa 2005 katika studio za FP Records chini ya uangalizi wa “Producer”  Fleva, huku akifichua kua show yake ya kwanza ya kutumbuiza mashabiki iliandaliwa katika mkahawa wa Happy Nights mjini Watamu.

Kwa sasa amekuja na kibao kipya kiitwacho “Machozi” akimshirikisha mwanadada kwa jina Shamim a.k.a Shamo, kilichoimbwa kwa lugha ya Kiswahili na kiarabu na kurekodiwa katika studio ya Bado Records, inayopatikana mjini Watamu katika kaunti ya Kilifi mkoani Pwani.

Mr. Bado afichua kuwa mwadada huyu kwa jina Shamim a.k.a Shamo ni dadake mdogo na ushirikiano huu ulikuwa wa kum’introduce kwa “game” ya Mombasani. Mr. Bado afichua kuwa familia yao imejaa wanamziki na mwadada huyu ni nduguye wa pili kujiunga na mziki baada ya kakake mkubwa Nyerere Juniour, ambaye ni msanii wa nyimbo za kitamaduni na babake Nyerer e Wa Konde.

Mr. Bado afichua kuwa karibuni anatarajia kusafiri ng’ambo na angependa kumwacha dadake mdogo akiendeleza ndoto ya mziki, ambayo amefichua kuwa ni sawa na urithi wa kifamilia.


Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.


MR. BADO & SHAMO - MACHOZI


Contacts:
http://www.facebook/Bado Mzungugiryama
badotalents@gmail.com


No comments:

Post a Comment