SEASON 2 YA BIFU KATI YA ANTIVIRUS(VINEGA) NA CLOUDS FM YAANZA
Uhasama kati ya mbunge wa mbeya Mjini nchini Tanzania Joseph
mbilinyi aka Mr. Two ( SUGU) na kituo kimoja cha redio nchini TZ (Clouds Fm)
unaoonekana kujichipuza tena.
Haya yanajiri wiki chache baada ya sugu na kundi lake la
wasanii waliotoa album mbili za kupaka matope kituo hichi na watangazaji wake (Anti
Virus vol 1 & 2 ) kupatanishwa na usimamizi wa kituo hicho chini ya waziri mmoja
wa serikali ya Tanzania.
Sugu na kundi lake walianzisha vita na kituo cha Clouds Fm – Radio ya
watu kufuatia madai ya nyimbo zao kutochezwa katika kituo hichi ambacho
kinaongoza nchini Tanzania
kwa waskilizaji na pia madai ya rushwa dhidi ya watangazaji wa kituo hicho.
Sugu na kundi lake wametuma ujumbe huu kwa vyombo vya habari, wakielezea
sababu ya kuanza tena kwa uahasama baina yao;
HAKIKA TUMEPITIA MENGI MACHUNGU NA HATUJAKATA TAMAA.JAMANI
TUELEWE JAMBO MOJA TU, NAFASI YA AMANI NDIO INAYOTAFUTWA POPOTE DUNIANI NA
KIZURI NI KWAMBA ADUI NDIO ANANYOOSHA MIKONO JUU KWA KUTAMBUA HARAKATI ZA MUZIKI
KWA VIJANA WA TAIFA HILI. TUMEKOMALIA MAMBO AMBAYO TUNAAMINI NDIO MIZIZI YA
UFISADI NA UKANDAMIZAJI WOTE UNAOFANYWA NA WAFU FM PAMOJA NA WANAOSHIRIKIANA
NAO (majina kwenye vol 3).
WAMECHOMOA NA KUYAKATAA MAKUBALIANO YOTE BAADA YA KUKUBALI
HAPO AWALI MBELE YA WAZIRI, KUPITIA KIKAO CHA UTEKELEZAJI WA MAKUBALIANO HAYO
MBELE YA VIONGOZI WA BASATA WALIOKUWEPO(ushahidi wa sauti za kikao upo na
tutautoa).
WAMEAMUA KUTURUDISHA VITANI NA HAYA NDIO MAISHA YETU.....NA
KILA MMOJA WETU ANASHANGAA JAMAA SIJUI NI NANI ANAYEWASHAURI KWANI WALILETA
SHAURI LA KUITWA MAHAKAMANI KWA WATU 7 AKIWEMO;
1. SUGU (aliyekamatwa mara kadhaa na kupelekwa makao makuu ya
usalama wa taifa,jukwaa la wahariri,police n.k)
2. DANI (anayetafutwa na aliyetishwa mara kadhaa n.k)
3. MKOLONI (aliyewahi kuwekewa sumu ili kuuwawa,aliyeenda
usalama,police,kwa Mh Waziri,anayetafutwa n.k)
4. RAMA D (anayetafutwa na ambaye nyumba yake iliingiliwa na
polisi usiku usiku n.k)
5. ADILI(ambaye alikamatwa na kupelekwa police central kwa
harakati hizi na watu bado tulisimama tukalimaliza)
NA SIO MAPACHA (wanaotafutwa n.k) PEKEE KAMA WATU
WANAVYODHANI NA TAARIFA HIZO SIJUI NI KARANI YUPI(mpumbavu) KAZIPELEKA BAR
INAITWA MLIMANI JIRANI NA ILIPO KAMBI YETU KAMPATIA MHUDUMU ANAITWA MAEDA.
ULIWAHI KUSIKIA WAPI KITU KAMA
HIKI?? ETI SUMMARCY ZA MAHAKAMA ZINAPELEKWA KWA COUNTER WA BAR?
Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.
No comments:
Post a Comment