Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Wednesday, March 21, 2012

JE MSANII JIMMIE GAIT NI “GAY?”






JIMMIE GAIT AKANA KUWA SHOGA

Msanii wa mziki wa injili nchini Jimmie Gait ameamua kuzima uvumi ambao kwa mda umesheheni katika mitandao ya kijamii, kuhusiana na "sexuality" yake, ambapo wengi wameelezea wasiwasi wao kwamba huenda akawa ni shoga.

Karibuni kumejitokeza mwanamume mmoja shoga ambaye amedai kwamba amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na msanii huyu wa nyimbo za injili.

Hata hivyo jimmie gait amejitokeza na kuweka wazi kwamba ana mchumba wa kike ambaye wame date kwa mda mrefu anayempenda sana na kuelezea kutoshangazwa kwake na uvumi huo kwani si mara ya kwanza maishani mwake amekuwa akifuatwa na mashoga waliotaka awe na uhusiano nao.

Gait pia aweka wazi kwamba hawachukulii vibaya wanaume mashoga na pia akaitaka jamii kuheshimu maisha yake yakibinafsi.

Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

No comments:

Post a Comment