Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Wednesday, March 21, 2012

NYIMBO MPYA YA MH. TEMBA KUTOKA APRIL






BAADA ya kumtoa Bi Cheka, msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka TMK, Mh Temba, amesema kuwa anatarajia kutoa ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Mazoea’, ambayo itatoka sambamba na video yake.

Msanii huyo ambaye amekuwa mstari wa mbele kuwatoa nyota chipukizi, asema wimbo huo ndiyo utakaokuwa wa kwanza kwa upande wake na anaamini utakuwa moto wa kuotea mbali.

 Alisema kuwa ngoma hiyo haitakuwa kuwa na mfano kwani muziki wake anafanya tofauti na wasanii wengine hivyo mashabiki wake wake mkao wa kula kuweza kuupokea ujio wake mpya.

“Hiyo ndo ngoma yangu mpya ambayo ambayo itakuwa sokoni April mwaka huu hivyo nawaomba mashabiki wangu wawe na uvumilivu kwani sitaki kufanya kitu kwa haraka baada nije kuharibu,” alisema..

Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

No comments:

Post a Comment