Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Wednesday, February 29, 2012

AVRIL AFICHUA UGUMU WA KUANDIKA NYIMBO YAKE MPYA



AVRIL

AVRIL AFICHUA UGUMU WA KUANDIKA “ KITU KIMOJA”

Mwimbaji Avril afichua kwamba idea ya kwanza ya melody ya wimbo wake mpya “Kitu kimoja” ilikataliwa na producer wake Lucas wa Ogopa DJ’S.

Avril asema Lucas alimpa challenge afanye wimbo mzuri kuhusu mapenzi na kumtaka amuandikie wimbo mtu asie na uwezo wa kuona.

Avril  asema Lucas alitaka wimbo atakao uandika umfanye kipofu afurahi na ajisikie kupendwa.

“Nilijaribu kuhepa hepa hii idea akaniambia hapana rudi hukuuuuu”

Avril ambaye ameanza ujenzi wa nyumba ya wazazi wake akitumia pesa za faida ya mziki wake, amesema “ili kupata idea ya kuandika huu wimbo ilinibidi nifunge macho na kuaanza kuiandika na maneno yakawa yanakuja tu”

Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

No comments:

Post a Comment