Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Sunday, February 26, 2012

MSANII WA MALINDI KLEANHEART ATOA WIMBO MPYA





KLEANHEART

Emmanuel Ogutu a.k.a Kleanheart ni msanii wa Hip Hop na R&B kutoka mji wa  Malindi {Chocolate City} ambaye alianza safari yake ya mziki mwaka wa 1997 akiwa katika kikosi cha “Akraba” wakiwemo na wasanii wengine “Jix” na “Mc Diddy.”

Amekuwa nyuma ya pazia ya muziki huku mashabiki wake wakiwa na hamu yakutakakujuwa chanzo cha kimya chake. Akifichua sababu yenyewe Kleanheart asme masomo yalikosa kumpa nafasi ya kushughulikia mziki hadi pale alipo maliza kidato cha nne mwaka wa 2006.

Ni mzaliwa wa mji wa Malindi Kisumu-Ndogo na alisomea shule ya msingi ya Malindi Primary school(HGM) kabla ya kupata elimu ya upili Kakuyuni Secondary. Hajaoa yupo “single” na ni mtoto wa tisa katika family ya Mama Nora Ogutu na Mzee Ogutu Atata babake ,ambaye ni marehemu kwa sasa.

Hali yake kama Mlemavu ni changamoto pia katika maisha yake ya kisanii japo ndoto zake ni kubwa na zinamuacha na matumaini mengi. Klean heart alidondosha vibao kama “Tabia za madem”, “Naitwa pesa,” “Nipe nafasi” na pia kushirikishwa katika kolabo mbalimbali kama “Take it slow,” aliyoifanya na msanii GRA, “Marina” ya msanii Musha, “Joy” ya msanii  Escobar miongoni mwa nyenginezo.

Ni mmiliki mkuu wa Heartland Films kampuni inayo shughulika na filamu na video za muziki mjini Malindi. Pia anahusika na utayarishi wa gazeti la kila mwezi ambalo karibu litakuwa nje kwa jina MTAZAMO MAGAZINE. 

Kwa sasa Kleanheart ametoa wimbo mpya kwa jina "CHEMCHEM ZA KISANII " ajia kutoka kwa albam yake ya pili kwa jina “AKILI KICHWANI".

Anawaomba mashabiki wamshike mkono katika safari ndefu ya muziki huku akiwaahidi mambo mapya kila uchao.

Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

No comments:

Post a Comment