Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Monday, February 20, 2012

CANNIBAL NA PREZZO KUJA MOMBASANI KUFANYA VIDEO:






“SCENES KADHAA ZA KATIKA VIDEO YA MY CITY MY TOWN ZITAKUWA ZA MOMBASA”

Msanii mkali wa mziki wa Mombasani Cannibal anakamailisha matayarisho ya ku’shoot video ya wimbo wake mpyao wa “My City my Town” aliomshirikisha msanii mkali wa Nairobi, Prezzo.

Akizungumza na Kaya Flavaz, Cannibal ambaye pamoja na Prezzo wanatengeneza kundi jipya la wanamziki nchini kwa jina MakiniMasaiMusic Group(MMMG) afichua kuwa, baadhi ya sehemu zitakazo tumiwa katika video hiyo zitakuwa jijini Mombasa hususan katika mistari inayotaja mkahawa wa Bellavista na hoteli ya Tarbush.

“Lazima kutakua na scenes za Mombasa kwa sababu huku Nairobi hakuna watoto wa kimanga wala wali wa nazi na biriani. Watu wa kujipaka hina wanapatikana Mombasani so itabidi tuje,” akasema.

Cannibal afichua kuwa atakuja Mombasa hivi karibuni ku’finalize kabla ya kurudi Nairobi na kushuka na mzee mzima Prezzo kwa shooting ya video.

Video shooting natumai itakua in the next two weeks lakini kabla hiyo time natarajia kuja Mombasa kukamilisha mipango kabla ya kurudi Nairobi halaf nishuke na Prezzo.

Cannibal pia afichua kuwa anapanga kufika Radiokaya kwa interview ndani ya show nambari moja mkoani pwani “Kaya Flavaz”.

Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

No comments:

Post a Comment