Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Sunday, February 19, 2012

MASHANGINGI YASUMBUA WASANII WA BONGO.


YOUNG D, DOGO JANJA NA DOGO ASLAY WASUMBULIWA NA MAJIMAMA

Makinda wa Bongo Fleva, David Genz Mwanjela ‘Young D’, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ na Aslay Isihaka ‘Dogo Aslay’ wadaiwa kusumbuliwa na mijimama kimapenzi huku baadhi yao wakidaiwa kuvuta bangi.

Baadhi ya wakereketwa wa sanaa ya Bongo Fleva  waomba wasani hawa wadogo wakatazwe mapema kujichanganya na tabia mbaya ambazo huenda zikahatarisha Maisha yao.

Msanii YOUNG D amabaye ana umri wa miaka 19 kwa sasa alikubali kwa kiwango flani Ukweli wa madia haya ya washikadau wa bongo flavaz. “Kusema kweli natongozwa na mijimama ila nina ‘girlfriend’ na kuhusu bangi, kimtindo si unaelewa? Hata hivyo, nakubali ushauri wa wadau ‘so’ nitakuwa makini.”


kwa upade wake msanii DOGO JANJA ambaye ana  umri wa miaka 15, aliwahi kukumbwa na scandal ya mapenzi alipokubali kutoroshwa usiku na mwanamke mmoja huku akidaiwa pia kuwa mtumizi wa bangi.
Hata hivyo akizungumzia madai haya Dogo Janja anayesoma kidato cha pili katika Shule ya Sekondari ya Makongo aliahidi kuwa makini zaidi.


kinda jipya kabisa katika mziki wa Bongo flavaz DOGO ASLAY ambaye pia ana umri wa miaka 15 na mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari ya Kata ya Tandika, Dar, anadaiwa kukumbana na usumbufu wa mijimama ya Dar.
Washikadau wa Bongo flavaz kwa sasa wanamtaka Said Fella ‘Mkubwa’ anayemlea kisanii Dogo Aslay kuwa makini.
Fella akubaliana na wadau kwamba kuna tabia amabazo dogo huyu anafaa kukatazwa.
“Naomba tusaidiane na jamii, siyo vizuri kumhusisha mtoto na mambo ya kikubwa kwani umri wake hauruhusu,” alisema Fella.


Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

No comments:

Post a Comment