Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Sunday, February 19, 2012


MSANII AMINI HUENDA AKAFUKUZWA THT!

Anakwenda kwa jina la Amini Mwinyimkuu ‘Amini’, taarifa ni kwamba msela huyu huenda akatimuliwa ndani ya kundi la ‘THT’, kutokana na utovu wa nidhamu.

Akiongea na mapema wiki hii Amini alisema kikubwa kinachotaka kumfukuzisha hapo ni kuchukia tabia za baadhi ya wasanii wa kundi hilo ambao wanajipendekeza kwa mabosi.

Hata hivi Amini alisema si kweli kuwa ana nidhamu mbovu kama inavyodaiwa lakini kutokana hulka yake ya kupenda kusimamia ukweli kwenye kila jambo basi amekuwa akionekana mkorofi.

Mpaka anaongelea swala hili uongozi wa THT ulikuwa unataka kukaa kikao kumjadili kwamba afukuzwe au abaki.

“Yani nimesikia kwamba najadiliwa na uongozi wa kundi ili niweze kufukuzwa lakini kwa upande wangu sioni kama ni tatizo kwa sababu kama kipaji ninacho hivyo nasema kama mimi ni mtovu wa ni nidhamu sawa niko tayari kuondoka,” alisema.


Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

No comments:

Post a Comment