Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Thursday, February 23, 2012

TUNAMKUMBUKA NA KUMUENZI SIR MALCOM P



Sir Malcom P
R.I.P SIR MALCOM P

Wakereketwa wa mziki Mombasani leo waadhimisha miaka miwili tangu kuondoka kwa msanii maarufu katika ukanda wa pwani Sir Malcom P.

Malcom P ambaye majina yake halisi ni Malcom Puga, alifariki siku kama ya leo mwaka wa 2010 kufuatia ajali mbaya ya barabarani katika barabara kuu ya Likoni - Lungalunga










Marehemu alikua ametoka nyumbani kwake Ukunda akielekea Kaloleni katika mkahawa mpya wa Kings ambako alikua anaenda kusherekea siku ya kuzaliwa kwake na alikuwa anafikisha miaka 35

Malcom P alikuwa meneja wa wa klabu ya Kings – Ukunda na Kings Recording studio na alikuwa amaefungua mkahawa mpya njini Kaloleni uliokuwa pia unaitwa Kings – Kaloleni.













Jumatano ya tarehe 24.02.2010 daima itabaki katika kumbukumbu za wakereketwa wa game ya Mombasani, kwani ni siku waliyompoteza kigogo wa game aliyekuwa ameshika mikono na kuwaenua wasanii na maproducer mbalimbali pwani, mbali na kufanya kazi zilizokubalika na wasanii wa taifa jirani la Tanzania.

Msanii Malcom P aliwahi kufanya kazi na kundi la TMK family, PNC na Yakuza Mobb.


Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

No comments:

Post a Comment