Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Sunday, March 11, 2012

BELLE9 APINGA KUIBA WIMBO WA SLIM G - NAJMA


BELLE9

BELLE9 APINGA KUIBA WIMBO WA SLIM G - NAJMA

Baada ya kusalia kimya kwa mda msaanii mkali nchini Tanzania Abednego Damien aka Belle9 ameamua kujibu madai yalioshamiri katika vyombo vya habari nchni Kenya, kwamba kuna wimbo alimuibia msanii kutoka Kenya kwa jina Slim G, wimbo unaojulikana kwa jina Najma.

Akizungumza na Kaya Flavaz jijini Dar Es Salaam, Belle9 asema  kuwa wimbo ambao unazungumziwa siwake na kufichua kuwa hajawahi kuimba wimbo kwa jina Najma. Belle9 asema kuna kipindi flani miaka ya nyuma aliwahi kusikia story kama hizo lakini baada ya ufuatilizi akagundua wimbo huo uliimbwa na msanii mwengine ambaye sauti yake imefanana sana na yake.

Belle9 asema tatizo hili limechangiwa na “pirates” ambao waliubatiza wimbo huu jina lake na kupelekea wimbo huo kusambaa ukiwa na jina la belle9 kupitia cybercafés zinazo burn mziki.

“Nyimbo zangu nilizoziimba mashabiki wangu wanazifahamu kutoka  na utunzi wa mashairi na style yangu kutoka enzi za Mapenzi ya sumu, Masogange We ni Wangu, Nilipe ni Sepe hadi sasa Nimerudi , ambayo ndio single yangu mpya” akasema Belle9.

“Kama hizi story ni kweli basi wangekuwa wamewahi kuniskia nikiu’peform wimbo huo.Lakini waliokuja kwa shows zangu Mombasa wanaweza kuwa mashahidi wangu. Sijawahi kuimba wimbo kama huo”.

Utafiti wa kayaflavaz wagundua kwamba original copy ya wimbo huu unaozungumziwa ulisave’iwa Kwa jina “NEIGHBOUR _-_NAJMA fullvision”. Na zaidi ya yote wimbo huu hauna "intro" wala "outro" inayotaja jina la studio wimbo ulikorekodiwa ama jina la msanii aliyeuimba, kinyume na nyimbo nyingi za wasanii wa kizazi kipya.

Belle9 hata hivyo hakuficha kughadhabishwa kwake na jinsi Slim G alivyoshughulikia utata huu  na kumlaumu kwa kuamua kwenda kwa media bila hata ya kuskia upande wa Belle9.

Zaidi ya yote Belle9 ashkuru Kaya Flavaz kwa kufanya juhudi za mchwa kumtafuta ili kuskia upande wake wa mtafaruku huu wote na kuelezea kushtushwa kwake na jinsi vituo kadhaa vya redio jijini Mombasa vilivyoshughulikia story hii.

Belle9 awaomba msamaha mashabiki wake kwa mtafaruku uliotokea na kufichua kwamba bado ataendelea kuwatumbuiza na nyimbo kali kali.

Hii si mara ya kwanza kwa “pirates” kulaumiwa katika kubadilisha majina ya nyimbo za wasanii. Itakumbukwa kwamba msanii Uncle Chonia  pia alijipata katika hali hii baada ya wimbo wake maarufu “Merimela” kusambaa na jina la msaniii Sudi Boy wa mombasani katika video.

Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

No comments:

Post a Comment