Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Friday, March 16, 2012

BIFU KATI YA ROMA MKATOLIKI NA IZZO BIZNESS


ROMA MKATOLIKI

BIFU KATI YA ROMA MKATOLIKI NA IZZO BIZNESS LANUKIA

Msanii mkali wa hip hop kutoka Mbeya nchini Tanzania Izzo Bizness aonekana kujiaanda kwa bifu dhidi ya rapper mwengine mkali katika ulimwengu wa Hiphop nchini Tanzania Roma Mkatoliki, baada ya kumshambulia kwa maneno akiwa jukwaani anaperform.

Izzo Bizness adai yeye yuko juu ya Roma Mkatoliki kimziki na kamwe hakuna hata siku moja atamfikia kimashairi.

“Roma ni mdogo sana kwangu na mimi ni mkubwa kwake, hii imekaa kihiphop kwa sababu kwenye hiphop kuna kupishana kauli kama hivyo”

Uhasama huu wakisanii waonekana kupigwa pondo na wasanii wengine baada ya Suma Lee kuweka wazi msimamo wake kuhusiana na hali ya kutofautiana kimziki kati ya wasanii hawa wawili.


Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

No comments:

Post a Comment