Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Thursday, June 14, 2012

AY KUFANYA VIDEO MBILI KWA MILIONI 6 AFRIKA KUSINI



AY
VIDEO MOJA ITAMGHARIMU KSH MILIONI 3.

Mwana mziki wa Bongo flava AY jumapili ya wikendi hii inayokuja anataajiwa kuvunja rekodi na kuwa mtanzania wa kwanza kuperform kwa mara ya pili kwenye stage ya Big Brother Africa.

Akizungumzia matayarisho yake AY afichua pia kuna uwezekano akaitumia fursa hiyo kufanya video yake pili.

Ni wiki mbili zimepita toka atoke Afrika Kusini alikokwenda kufanya video yake ya kwanza iliyomgharimu KSH milioni 3 iliyofanya na kampuni ya Godfather, ambayo imefanya video nyingi za P Square, J Martins, Mr Flavour na wengine.

Akizungumzia hatua yake ya kutumia fedha nyingi kwa video zake, AY asema “hii ni biashara na biashara yoyote ni lazima uwekeze hakuna faida inayokuja tu bure bure, watu ni uoga tu ujue wa kuwekeza wanabaki kuelekeza vidole kwa Wanigeria ambao wanawekeza pesa kwenye muziki, mimi najibana pia ninachokipata nakigawa.. hata zamani ilikua hivi hivi tu watu walikua wanashangaa Ay unakwenda Uganda unapoteza hela, leo hii wao wanahangaika kwenda Uganda na Kenya mimi nimeshatoka huko”

AY anatarajiwa kuondoka bongo jumamosi hii kwenda nchini afrika kusini kuperform katika show ya Big Brother siku ya jumapili akipanda stage moja na wakali wetu wa Kenya Sauti Sol.

Kwa mengi Zaidi usikose kuskiza "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™. 9AM - 1PM      (MON - FRI)


No comments:

Post a Comment