Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Wednesday, June 20, 2012

DIAMOND ANUNUA GARI LA KSH 3.1 MILLION

DIAMOND PLATINUMZ
DIAMOND ANUNUA GARI JIPYA:
Staa wa muziki wa kizazi kipya nchini Tz kwa sasa anayepeta zaidi Naseeb Abdul ‘Diamond  Platinumz’ amenunua gari jipya lenye thamani ya shilingi milioni 3.1 pesa za Kenya ama za Tsh 60,00000(milioni 60)

Gari hilo ni aina ya Land Cruiser Prado TX 2006 na alilipokea rasmi kutoka kwa wakala aliyekuwa akishughulikia mpango mzima  wa  kuliingiza Bongo.
LAND CRUISER PRADO TX 2006
Akifichua hayo mda mfupi baada ya kupokea  gari hilo Diamond asema amekua na mipango ya kumiliki gari design hiyo lakini kulikua na mambo kadhaa ambayo alkua anapanga kukamilisha kabla ya kununua gari hilo.

Kwa mengi Zaidi usikose kuskiza "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.9AM - PM. MON-FRI



Monday, June 18, 2012

WASANII KULIPA USHURU:



HUENDA WASANII WAKAANZA KULIPA USHURU:
Huenda wasanii nchini wakaanza kulipa ushuru iwapo pendekezo la waziri wa feedha nchini Robinson Githae litaratibishwa na kuwa sheria nchini.

Katika bajeti yae wiki iliyopita waziri huyu alipendekeza wasanii wano piga show kulipa asilimia 16 ya ushuru kutoka kwa hela wanazopata wanapo tumbuiza watu katika mikahawa mbali mbali.

Haya yanajiri huku wasnii nchinikenya wakiendelea kutia kibindoni hela zote wanazo lipwa kufuatia ukosefu wa sheria ya kuhakikisha wanalipa ushuru kama wafanyavyo wasnii katika mataifa mengine.

Hivi karibuni msanii R. Kelly nchini Marekani amejipata matatani  baada ya kugunduliwa kwamba hajakuwa akilipa ushuru kama inavyotakikana kwa miaka mingi.

Je wasanii wetu Mombasani wakotayari kulipa ushuru?

Je,  hela wanazopata katika mashow zinastahili kukatwa ushuru?

Kwa mengi Zaidi usikose kuskiza"Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.               9AM - 1PM      (MON - FRI)

OCTOPIZZO KUANZA BIASHARA YA CONDOM:


OCTOPIZZO
OCTOPIZZO ANAPANIA KUANZISHA “BRAND” YA CONDOM:
Msanii chipkizi jijini Nairobi anayetamba kwa sasa kwa jina Octopizzo afichua kuwa anamipango ya ku’launch ‘brand’ yake ya aina ya ‘Condom’ nchini.

Katika mahojiano na kitupo kimoja cha TV jijini Nairobi, Octopizzo asema ‘brand’ yake ya ‘condom’ itakua na ‘condom’ nne katika ‘Pack’ moja ‘instead ‘ya tatu kama ‘brand’ zegine za ‘condom’ nchini.(Duh!!!)
CONDOM
Hatua ya msanii huyu haitakuwa geni katika ulimwengu wa mziki wa kizazi kipya, kwani kuna wasanii wakubwa ulimwenguni ambao wameanzisha biashara ambazo haziambatani na mziki wao.

Mfano 50cent anakampuni ya maji ya ‘Vitamins’ huku msanii kama ‘Jay Z’ mbali na nguo akimiliki hisa katika klabu ya ‘New York Mets’  ya mchezo wa vikapu nchini Marekani.

Je ndoto hizi zitatimia?

Kwa mengi Zaidi usikose kuskiza "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.
9AM - 1PM      (MON - FRI)

Thursday, June 14, 2012

AY KUFANYA VIDEO MBILI KWA MILIONI 6 AFRIKA KUSINI



AY
VIDEO MOJA ITAMGHARIMU KSH MILIONI 3.

Mwana mziki wa Bongo flava AY jumapili ya wikendi hii inayokuja anataajiwa kuvunja rekodi na kuwa mtanzania wa kwanza kuperform kwa mara ya pili kwenye stage ya Big Brother Africa.

Akizungumzia matayarisho yake AY afichua pia kuna uwezekano akaitumia fursa hiyo kufanya video yake pili.

Ni wiki mbili zimepita toka atoke Afrika Kusini alikokwenda kufanya video yake ya kwanza iliyomgharimu KSH milioni 3 iliyofanya na kampuni ya Godfather, ambayo imefanya video nyingi za P Square, J Martins, Mr Flavour na wengine.

Akizungumzia hatua yake ya kutumia fedha nyingi kwa video zake, AY asema “hii ni biashara na biashara yoyote ni lazima uwekeze hakuna faida inayokuja tu bure bure, watu ni uoga tu ujue wa kuwekeza wanabaki kuelekeza vidole kwa Wanigeria ambao wanawekeza pesa kwenye muziki, mimi najibana pia ninachokipata nakigawa.. hata zamani ilikua hivi hivi tu watu walikua wanashangaa Ay unakwenda Uganda unapoteza hela, leo hii wao wanahangaika kwenda Uganda na Kenya mimi nimeshatoka huko”

AY anatarajiwa kuondoka bongo jumamosi hii kwenda nchini afrika kusini kuperform katika show ya Big Brother siku ya jumapili akipanda stage moja na wakali wetu wa Kenya Sauti Sol.

Kwa mengi Zaidi usikose kuskiza "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™. 9AM - 1PM      (MON - FRI)


DRAKE APIGANA NA CHRIS BROWN


CHRIS BROWN
Taarifa kutoka nchini Marekani zadai kuwa msanii kwa jina Drake kutoka kundi la YMCMB amepigana na msanii wa mwengine wa RnB nchini kwa jina Chris Brown.
DRAKE
Taarifa hizo zadai wasanii hao walkutana katika klabu moja usiku jiji New York . inadia msanii Chris Brown alinunua Champagne  na kumtuma mmoja wa wahudumu wa klabu hiyo kupelekea kinyaji hicho kwa meza ya akina Drake lakini msanii Drake akamua kurudisha kinywaji hicho pamoja na ujumbbe katika kikaratasi ( “I’m F******* the love of your life) akimaanisha msanii wa kike Rihanna.

Ghafla bin vu vuramai likazuka na jamaa hawa wawili wakaamua kuzichapa kavu kavu bila gloves za boxing.
KIDEVU CHA CHRIS BROWN BAAD AYA VURUMAI
Kwa mengi Zaidi usikose kuskiza "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™. 9AM - 1PM      (MON - FRI)



DOGO JANJA AFURUSHWA NA MADEE

DOGO JANJA
DOGO JANJA ARUDI KWAO ARUSHA BAADA YA KUKOSANA NA MADEE.


Msanii Madee wa Tip Top Connection ambae ndio alikabidhiwa na wazazi kumlea na kumsimamia Dogo Janja azungumzia sababu zake za kumrudisha Dogo Janja mikononi mwa wazazi wake.

Madee asema ameshindwa kuishi na Dogo Janja.

Madee asema Dogo Janja aliekua form II katika shule ya Makongo High School amekataa kusoma na hawezi kukaa nae wakati hataki kusoma.

Madee afichua kuwa juzi alkua safarini Iringa na Mbeya na aliporudi mwalimu wa Dogo Janja limpigia simu na kumpa pole kwa sababu Dogo Janja anaumwa. Hata hivyo alipofika nyumbani akampata Dogo Janja akiwa mzima wa afya lakini kakataa kwenda shule na kudaganya ni mgonjwa.

DOGO JANJA AKIWA STENDI YA BASI ASUBUHI YA LEO
Baada ya malumbano, akamuuliza ka anataka kusoma au kuzurura mtaani? Dogo akajibu kwamba anataka kwenda kusoma kwaoArusha badala ya sas Dar Es Salaam, ikabidi ampigie simu baba yake palepale ambapo mzee wake aligahiri na kumuomba Madee asimrudishe Arusha  bali aendelee kukaa nae Dar.

Hata hivyo baadaye Madee alichukua simu ya dogo na akagundua vitu vingi sana vya kishenzi shenzi vilvyoandikwa kumhusu. Baada ya malumbano zaidi Dogo akakita palepale anataka kurdi Arusha na Madee akampa baraka zote.
DOGO JANJA NDANI YA BASI


Dogo kaondoka leo Asubuhi kuelekea kwao Arusha….. Swali je twajifunza nini hapa?
Kwa mengi Zaidi usikose kuskiza "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™. 9AM - 1PM      (MON - FRI)