Kaya Flavaz

Kwa Uhondo Wa Habari Za Sanaa Ya Mombasani.

Wednesday, March 28, 2012

NYOTA NDOGO AACHILIA VIDEO YA WIMBO "MOYO"


NYOTA NDOGO


NYOTA ACHILIA VIDEO YA WAIMBO WAKE "MOYO".


Msanii mkali wa kike kutoka Mombasa Nyota Ndogo anatarajiwa kuachilia video ya  single yake inayojulikana kama "Moyo"baadaye leo jioni katika kipindi cha Mambo Mseto.


Akizungumza na Kaya Flavaz, Nyota ndogo asema video hiyo imechelewa kiasi lakini kwa sasa imekamilika na mashabiki wake wataiona kwa sana hivi karibuni.


Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

Wednesday, March 21, 2012

BOB JUNIOR KUACHILIA VIDEO YA WIMBO MPYA KABLA YA AUDIO





BOB JUNIOR KUACHILIA VIDEO HALAFU BAADAYE AUDIO YA WIMBO WAKE MPYA "NIMCHUMU"

Msanii mkali wa mziki wa Bongo fleva ambaye pia ni producer Bob Junior, afichua kuwa anapanga kuachilia video ya wimbo wake mpya kwa jina “Nichumu” kwanza kabla ya kusambaza "audio" kwa vituo vya redio



Akizungumzia wimbo huo, msanii/producer huyo adai kuwa katika ngoma hiyo ameimba zaidi kuliko nyimbo zote alizowahi kuzitoa na anaamini mashabiki wa bongo fleva watakapouskia hawatachoka kuuskiza tena na tena.



Bob Juniour asema kikubwa alichokiimba ndani ya kazi hiyo ni mapenzi ambayo anaamini hayana kikomo na mwisho wa kupenda ni pale mungu atakapokuchukua.



“Hakuna asiyejua raha ya kupendwa hivyo hii ni ngoma ambayo imejaa mapenzi na naamini  mashabiki wangu wataipenda kutokana na ubora wake,” alisema.


Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

NYIMBO MPYA YA MH. TEMBA KUTOKA APRIL






BAADA ya kumtoa Bi Cheka, msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka TMK, Mh Temba, amesema kuwa anatarajia kutoa ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Mazoea’, ambayo itatoka sambamba na video yake.

Msanii huyo ambaye amekuwa mstari wa mbele kuwatoa nyota chipukizi, asema wimbo huo ndiyo utakaokuwa wa kwanza kwa upande wake na anaamini utakuwa moto wa kuotea mbali.

 Alisema kuwa ngoma hiyo haitakuwa kuwa na mfano kwani muziki wake anafanya tofauti na wasanii wengine hivyo mashabiki wake wake mkao wa kula kuweza kuupokea ujio wake mpya.

“Hiyo ndo ngoma yangu mpya ambayo ambayo itakuwa sokoni April mwaka huu hivyo nawaomba mashabiki wangu wawe na uvumilivu kwani sitaki kufanya kitu kwa haraka baada nije kuharibu,” alisema..

Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

BLACKFELLA'S NEW VIDEO IS OUT


COAST'S HIPHOP MOGUL BLACKFELLA RELEASED A NEW VIDEO





LISTENED TO THIS HIP HOP JOINT FROM BONGO...THESE GUYS KILLED IT ON THE BEAT, FLOW & CHORUS



BIFU KATI YA SUGU NA CLOUDS FM LARUDI TENA


MR TWO

SEASON 2 YA BIFU KATI YA ANTIVIRUS(VINEGA) NA CLOUDS FM YAANZA

Uhasama kati ya mbunge wa mbeya Mjini nchini Tanzania Joseph mbilinyi aka Mr. Two ( SUGU) na kituo kimoja cha redio nchini TZ (Clouds Fm) unaoonekana kujichipuza tena.

Haya yanajiri wiki chache baada ya sugu na kundi lake la wasanii waliotoa album mbili za kupaka matope kituo hichi na watangazaji wake (Anti Virus vol 1 & 2 ) kupatanishwa na usimamizi wa kituo hicho chini ya waziri mmoja wa serikali ya Tanzania.

Sugu na kundi lake walianzisha vita na kituo cha Clouds Fm – Radio ya watu kufuatia madai ya nyimbo zao kutochezwa katika kituo hichi ambacho kinaongoza nchini Tanzania kwa waskilizaji na pia madai ya rushwa dhidi ya watangazaji wa kituo hicho.

Sugu na kundi lake wametuma ujumbe huu kwa vyombo vya habari, wakielezea sababu ya kuanza tena kwa uahasama baina yao;


HAKIKA TUMEPITIA MENGI MACHUNGU NA HATUJAKATA TAMAA.JAMANI TUELEWE JAMBO MOJA TU, NAFASI YA AMANI NDIO INAYOTAFUTWA POPOTE DUNIANI NA KIZURI NI KWAMBA ADUI NDIO ANANYOOSHA MIKONO JUU KWA KUTAMBUA HARAKATI ZA MUZIKI KWA VIJANA WA TAIFA HILI. TUMEKOMALIA MAMBO AMBAYO TUNAAMINI NDIO MIZIZI YA UFISADI NA UKANDAMIZAJI WOTE UNAOFANYWA NA WAFU FM PAMOJA NA WANAOSHIRIKIANA NAO (majina kwenye vol 3).

WAMECHOMOA NA KUYAKATAA MAKUBALIANO YOTE BAADA YA KUKUBALI HAPO AWALI MBELE YA WAZIRI, KUPITIA KIKAO CHA UTEKELEZAJI WA MAKUBALIANO HAYO MBELE YA VIONGOZI WA BASATA WALIOKUWEPO(ushahidi wa sauti za kikao upo na tutautoa).

WAMEAMUA KUTURUDISHA VITANI NA HAYA NDIO MAISHA YETU.....NA KILA MMOJA WETU ANASHANGAA JAMAA SIJUI NI NANI ANAYEWASHAURI KWANI WALILETA SHAURI LA KUITWA MAHAKAMANI KWA WATU 7 AKIWEMO;

1. SUGU (aliyekamatwa mara kadhaa na kupelekwa makao makuu ya usalama wa taifa,jukwaa la wahariri,police n.k)
2. DANI (anayetafutwa na aliyetishwa mara kadhaa n.k)
3. MKOLONI (aliyewahi kuwekewa sumu ili kuuwawa,aliyeenda usalama,police,kwa Mh Waziri,anayetafutwa n.k)
4. RAMA D (anayetafutwa na ambaye nyumba yake iliingiliwa na polisi usiku usiku n.k)
5. ADILI(ambaye alikamatwa na kupelekwa police central kwa harakati hizi na watu bado tulisimama tukalimaliza)

NA SIO MAPACHA (wanaotafutwa n.k) PEKEE KAMA WATU WANAVYODHANI NA TAARIFA HIZO SIJUI NI KARANI YUPI(mpumbavu) KAZIPELEKA BAR INAITWA MLIMANI JIRANI NA ILIPO KAMBI YETU KAMPATIA MHUDUMU ANAITWA MAEDA.

ULIWAHI KUSIKIA WAPI KITU KAMA HIKI?? ETI SUMMARCY ZA MAHAKAMA ZINAPELEKWA KWA COUNTER WA BAR?

KWA HIYO TUNAWAOMBA WATANZANIA WOTE KWA UJUMLA WAELEWE KUWA CLOUDS FM WAMETURUDISHA VITANI RASMI NA KWA UFUPI TUPO KAMBINI WATAHUSUDU..................VOL 3 COMING OUT SOON!!!!!!


Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

JE MSANII JIMMIE GAIT NI “GAY?”






JIMMIE GAIT AKANA KUWA SHOGA

Msanii wa mziki wa injili nchini Jimmie Gait ameamua kuzima uvumi ambao kwa mda umesheheni katika mitandao ya kijamii, kuhusiana na "sexuality" yake, ambapo wengi wameelezea wasiwasi wao kwamba huenda akawa ni shoga.

Karibuni kumejitokeza mwanamume mmoja shoga ambaye amedai kwamba amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na msanii huyu wa nyimbo za injili.

Hata hivyo jimmie gait amejitokeza na kuweka wazi kwamba ana mchumba wa kike ambaye wame date kwa mda mrefu anayempenda sana na kuelezea kutoshangazwa kwake na uvumi huo kwani si mara ya kwanza maishani mwake amekuwa akifuatwa na mashoga waliotaka awe na uhusiano nao.

Gait pia aweka wazi kwamba hawachukulii vibaya wanaume mashoga na pia akaitaka jamii kuheshimu maisha yake yakibinafsi.

Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

Friday, March 16, 2012

KLEANHEART ACHILIA VIDEO YA WIMBO "CHEMCHEM ZA KISANII"




KLEANHEART
KLEANHEART ACHILIA VIDEO MPYA.

Siku chache baada ya msanii mkali kutoka Malindi(Choclate City) Kleanheart kuachilia wimbo wake mpya kwa jina "Chemchem Za Kisanii", msanii huyo a'release official video ya wimbo huo.

Kleanheart ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Heartland Films iliyoko mjini Malindi afichua kuwa huu ndio mwanzo tu wa mabo mazuri kutoka kwake kama msanii.

Kleanheart pia afichua uwepo wa harakati za kuibua kundi la wasanii wakali kutoka mjini Malindi kupitia project ya "Starlent," ambayo inalenga kuinua wasanii wenye malengo ya kufanikiwa kimziki na kuuweka mji wa Malindi katika ramani ya mziki wa "Ngomapwani"



Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

BIFU KATI YA ROMA MKATOLIKI NA IZZO BIZNESS


ROMA MKATOLIKI

BIFU KATI YA ROMA MKATOLIKI NA IZZO BIZNESS LANUKIA

Msanii mkali wa hip hop kutoka Mbeya nchini Tanzania Izzo Bizness aonekana kujiaanda kwa bifu dhidi ya rapper mwengine mkali katika ulimwengu wa Hiphop nchini Tanzania Roma Mkatoliki, baada ya kumshambulia kwa maneno akiwa jukwaani anaperform.

Izzo Bizness adai yeye yuko juu ya Roma Mkatoliki kimziki na kamwe hakuna hata siku moja atamfikia kimashairi.

“Roma ni mdogo sana kwangu na mimi ni mkubwa kwake, hii imekaa kihiphop kwa sababu kwenye hiphop kuna kupishana kauli kama hivyo”

Uhasama huu wakisanii waonekana kupigwa pondo na wasanii wengine baada ya Suma Lee kuweka wazi msimamo wake kuhusiana na hali ya kutofautiana kimziki kati ya wasanii hawa wawili.


Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

DIAMOND KUIMBA TAARAB


DIAMOND
DIAMOND AFIKIRIA KUBADILI STYLE YA MZIKI HADI TAARAB


Naseeb Abdul aka Diamond msanii anayevuma kwa sasa nchini Bongo afichua kuwa anafikiria kubadili style ya nyimbo zake nakuingilia mtindo wa taarabu.


Diaomond asema haya yanamfika akilini mwake baada ya kukosa mpinzani kwenye style ya bongo fleva nchini Tanzania.


Diamond asema katika maisha yake ya kimziki hakuna msanii ambaye anaweza kufikia kiwango chake kisanii . Diamond ataja hatua ya nyimbo zake kuhit bila ya kumshirikisha msanii mwengine kama inshara mojawapo ya ukali wake katika ulimwengu wa Bongo flevaz.


Diamond asema kinachomfanya kufikiria kufanya kila aina ya muziki ni kipaji alichonacho, kwani  anaamini kuwa hashindwi na chochote kufuatia uwezo wake wa kisanii.


Msanii huyo aongeza kuwa bado hajaamua kufanya muziki huo rasmi lakini anafikiria kama unaweza kumletea soko kama ilivyo mziki wa bongo fleva, ambao umemfanya ajulikane duniani kote.


Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

Sunday, March 11, 2012

BELLE9 APINGA KUIBA WIMBO WA SLIM G - NAJMA


BELLE9

BELLE9 APINGA KUIBA WIMBO WA SLIM G - NAJMA

Baada ya kusalia kimya kwa mda msaanii mkali nchini Tanzania Abednego Damien aka Belle9 ameamua kujibu madai yalioshamiri katika vyombo vya habari nchni Kenya, kwamba kuna wimbo alimuibia msanii kutoka Kenya kwa jina Slim G, wimbo unaojulikana kwa jina Najma.

Akizungumza na Kaya Flavaz jijini Dar Es Salaam, Belle9 asema  kuwa wimbo ambao unazungumziwa siwake na kufichua kuwa hajawahi kuimba wimbo kwa jina Najma. Belle9 asema kuna kipindi flani miaka ya nyuma aliwahi kusikia story kama hizo lakini baada ya ufuatilizi akagundua wimbo huo uliimbwa na msanii mwengine ambaye sauti yake imefanana sana na yake.

Belle9 asema tatizo hili limechangiwa na “pirates” ambao waliubatiza wimbo huu jina lake na kupelekea wimbo huo kusambaa ukiwa na jina la belle9 kupitia cybercafés zinazo burn mziki.

“Nyimbo zangu nilizoziimba mashabiki wangu wanazifahamu kutoka  na utunzi wa mashairi na style yangu kutoka enzi za Mapenzi ya sumu, Masogange We ni Wangu, Nilipe ni Sepe hadi sasa Nimerudi , ambayo ndio single yangu mpya” akasema Belle9.

“Kama hizi story ni kweli basi wangekuwa wamewahi kuniskia nikiu’peform wimbo huo.Lakini waliokuja kwa shows zangu Mombasa wanaweza kuwa mashahidi wangu. Sijawahi kuimba wimbo kama huo”.

Utafiti wa kayaflavaz wagundua kwamba original copy ya wimbo huu unaozungumziwa ulisave’iwa Kwa jina “NEIGHBOUR _-_NAJMA fullvision”. Na zaidi ya yote wimbo huu hauna "intro" wala "outro" inayotaja jina la studio wimbo ulikorekodiwa ama jina la msanii aliyeuimba, kinyume na nyimbo nyingi za wasanii wa kizazi kipya.

Belle9 hata hivyo hakuficha kughadhabishwa kwake na jinsi Slim G alivyoshughulikia utata huu  na kumlaumu kwa kuamua kwenda kwa media bila hata ya kuskia upande wa Belle9.

Zaidi ya yote Belle9 ashkuru Kaya Flavaz kwa kufanya juhudi za mchwa kumtafuta ili kuskia upande wake wa mtafaruku huu wote na kuelezea kushtushwa kwake na jinsi vituo kadhaa vya redio jijini Mombasa vilivyoshughulikia story hii.

Belle9 awaomba msamaha mashabiki wake kwa mtafaruku uliotokea na kufichua kwamba bado ataendelea kuwatumbuiza na nyimbo kali kali.

Hii si mara ya kwanza kwa “pirates” kulaumiwa katika kubadilisha majina ya nyimbo za wasanii. Itakumbukwa kwamba msanii Uncle Chonia  pia alijipata katika hali hii baada ya wimbo wake maarufu “Merimela” kusambaa na jina la msaniii Sudi Boy wa mombasani katika video.

Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.

Wednesday, March 7, 2012

MSANII WA BONGO AJIPA NA MSANII WA KENYA



BABY MADAHA
BABY MADAHA AJIPA NA KIFUA CHA NAMELESS

NYOTA wa muziki anayetingisha pia kwenye anga la filamu za Kibongo, Baby Joseph Madaha (pichani) amefunguka kuwa nafasi aliyopewa ya kukilalia kifua cha mwanamuziki, David Mathenge ‘Nameless’ alipozuru Bongo hivi karibuni, imemfanya achizike na kuikumbuka hadi leo.

Baby Madaha afichua kuwa walipeana mda wa kutosha kiasi ambacho kinamfanya amkumbuke  Nameless.

“ninawasiliana naye kwa mtandao wa Facebook kwa kweli nilijisikia freshi sana  wakati nilipokilalia kifua chake pale jukwaani,”

Hata hivyo, Baby Madaha asema uhusiano wake na Nameless ni  wakawaida wala haujavuka…mpaka.

Monday, March 5, 2012

JOSE CHAMELEONE AFUNGUA KAMPUNI YA SIMU



JOSE CHAMELEONE:

Msanii mkali nchini Uganda Jose Chameleone amefungua kampuni mpya ya simu za rununu.

Inaripotiwa kwamba Chameleone anaagiza simu za rununu kutoka nchini China na atakua anazisambaza nchini Uganda.

Kulingana na habari kutoka nchini Uganda simu hizo ambazo zitaitwa kwa jina “Chameleone Phone” zitakuwa na rangi tofauti tofauti mithili ya kinyonga.

Msanii huyo afichua mauzo ya simu hizo za “Chameleone” yanatarajiwa kuanza mwezi wa Aprili

Thursday, March 1, 2012

JE “BIFU” ZINASAIDIA WASANII?



JE “BIFU” ZINASAIDIA WASANII?

Historia ya muziki wa kizazi kipya haiwezi kukamilika pasipo kutaja matukio ya uhasama kati ya baadhi ya wasanii wa muziki huo.Pengine neno ‘uhasama’ halileti ladha ama kuzua hisia zaidi katika ulimwengu wa mziki wa kizazi kipya.Neno ‘bifu’, linalotokana na ‘beef’ ambalo ni slang ya Kiingereza cha Wamarekani  Weusi, ni neno ambalo wengi hulitumia kuashiria uhasama kati ya wanamziki hususan wa kizazi kipya hapa mombasani.

Mwandishi mmoja wa gazeti la Daily Mail la Uingereza aliwahi kuandika kuwa ‘vituko katika fani ya muziki wa hip-hop na rap ni miongoni mwa chembechembe muhimu kwa mafanikio ya msanii wa muziki huo’. Alitaja vituko hivyo kuwa ni pamoja na bifu. Iwapo bifu zinasaidia uhai wa hip-hop na rap au zinadidimiza, mie sina jibu bali kwa namna moja au nyingine zimewasaidia baadhi ya wasanii kufanya vizuri katika mauzo ya albamu zao.

Katika mjadala wa kubainisha iwapo bifu ama uhasama baina ya wasanii husadia ama kutosaidia kukua kwa sanaa ya mziki mombasani, washikadau wakuu wa mziki wa kizazi kipya (mashabiki) wachora mitazamo tofauti.


WALIOUNGA MKONO.

Katika Kipindi cha Chipkizi Za Kaya Jumapili iliyopita Walioegemea mtazamo kwamba bifu husaidia wa hoji kwamba tabia ya uhasama baina ya wasanii ni utamaduni wajadi hususan katika ulimwengu wa mziki wa Hiphop. Uhasama huu watajwa kuongeza umaarufu wa wasanii husika kwani waskilizaji hugawanyika na kuamua ni yupi kati ya wasanii wawili wanaolumbana watawashabikia. Hii huzua na kujenga mashabiki sugu wa wasanii husika, ambao wanaweza kufananishwa na mashabiki sugu wa timu za soka. Kuna imani miongoni mwa baadhi ya wapenzi wa hip-hop na rap kwamba bifu kati ya wasanii marehemu Tupac Shakur na Notorious B.I.G ilisaidia sana kuongeza umaarufu wa wasanii hao.

Bila shaka wafuatiliaji wa bongoflava wanakumbuka bifu kati ya Juma Nature na Inspekta Haroun na ile ya wasanii wa East Coast Team na wale wa maeneo ya Temeke. Japo haifahamiki vizuri historia ya bifu hizo mbili, lakini kwa hakika zilivuta hisia za wapenzi wengi wa bongoflava.Hapa mombasani mbali na kupanda kwa joto la kisiasa mwaka wa 2007 uhasama kati ya wasaani waliokua juu nyakati hizo Rudeboys na msanii aliyekua anachipuka Susumila yatajwa kuchangia kupanda kwa umaarufu wa Susumila miongoni mwawakereketwa wa fani ya Mombasani. Jijini Nairobi kupanda kwa umaarufu wa Octopizzo watajwa kuchangiwa sana na uhasama baina yake na msanii mkongwe wahiphop Abbas Kubaff, huku bifu kati ya Bamboo na wafuasi wa kundi la Klepto pia latajwa kuchangia kutambulika kwa baadhi ya wasanii wa kundi hilo.
Tabia hii pia yatajwa kuongeza mauzo ya album katika mataifa yaliyoendelea. Bifu kati ya msanii Rick Ross na 50 Cent nchini marekani inaaminika kuchangia mauzo mazuri ya albmu ya Rick Ross inayofahamika kama ‘Deeper Than Rap‘.

Hata hivyo,kama kweli bifu zinasaidia maendeleo ya wasanii, kwanini basi marapa kama Ja Rule na Fat Joe ‘wamepotea’ licha ya bifu lao na 50 Cent huku Benzino akibaki historia baada ya bifu lake na Eminem?Au ili bifu lizae matunda ‘yanayokusudiwa’ sharti wahusika ‘waimudu’(kama Rick Ross alivyoweza ‘kustahimili’ bifu lake na 50 Cent)?Lakini kama suala ni ‘kumudu bifu’ mbona Jadakiss ameweza ‘kusimama vizuri’ hata baada ya ‘kupatana’ na 50 Cent?

Wakichangia mjadala huu katika kipindi cha Chipkizi za Kaya, baadhi ya wasikilizaji pia wasema amani haiji ila kwa ncha ya upanga na kinachofuata baada ya uhasama huu  huwa mapatano na heshima. Uwepo wa heshma katika sanaa ya mziki kunachangia kukua kwa mziki kwani mipaka baina ya wasanii mbali mbali huwa wazi na kazi zao ndizo zinazowawakilisha kwa mashabiki wao.

WALIOPINGA;
Msemo wa umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu ulikua kauili mbiu ya wengi waliopinga kwamba uhasama husaidia sanaa ya mziki wa kizazi kipya. Bifu yatajwa kuleta mgawanyiko si kwa wasanii wahusika pekee, bali hata kwa mashabiki. Hali hii yatajwa kusabaratisha baadhi ya wasanii na kupeana nafasi kwa wasanii wachache kupata mafanikio ya kimziki pekee kwa mda mrefu.

Kusambaratika kwa kundi la ECT na TMK baada ya bifu yao kwatajwa kama mfano. Bifu kati ya wasanii wa iliyokuwa East Coast Team na wale wa Temeke ilikufa kitambo kama ilivyotokea kwa bifu kati ya Nature na Inspekta. Lakini cha kushangaza, sio tu kwamba bifu hizo zilikwisha bali pia kulijitokeza mabadiliko makubwa kuhusu wasanii waliohusika na bifu hizo.

East Coast Team ilisambaratika huku wanakundi MwanaFA na AY wakitangaza kufanya kazi zao za kisanii kibinafsi (na wameendelea kuwa na mafanikio makubwa) lakini majina kama King Crazy GK (kiongozi wa kundi hilo) na O’Ten yamebaki kuwa historia tu.Kwa wenzao wa Temeke, japo kulizuka bifu jingine kati ya Wanaume Family na Wanaume Halisi baada ya kundi la Wanaume kugawanyika, kinachoweza kupigiwa mstari zaidi ni ‘kupotea’ kwa Nature na Inspekta katika anga za bongofleva.Ikumbukwe kuwa wasanii hao wawili walifikia hatua ya kupatana bbadaye na kushirikiana katika kundi la Wanaume Halisi.

Wanaoshuku mtazamo kwamba bifu hupelekea kupanda kwa mauzo ya album za wasanii wahusika wapiga mfano wa kudorora kwa mauzo ya album ya 50 Cent ya ‘Before I Self Destruct‘  licha ya uwepo wa bifu kubwa na msanii mwengine Rick Ross?

Udogo wa game ya Mombasani pia watajwa kutoweza kuwafanikisha wasanii wenye bifu. Uchache wa mashabiki wazua ugumu wa kuwaganya kwani hata wakigawanywa wale ambao msanii atawapata hawawezi kumfaidisha.Kutokuwa na utamaduni wa mashabiki kununua album madukani ama kupitia mtandao pia kwatajwa kutowafaidisha wenye bifu kwani uhasama wao hutajwa tu maredioni na hakutakua na faida kwao. Pia mashabiki wasema Ifikiapo hapa huhitajika utayari wa washikadau wa vyombo vya habari kuzungumzia bifu hili kuwafikia mashabiki lakini isipokuwa hivi, bifu hili huishia mitaani likijulikana na wasanii wenyewe tu na marafikizao wa karibu.

Wengine wasema ili ufanisi upatikane kutokana na bifu, kunahaja ya wasanii wote kuhusika vilivyo katika uhasama huo. Msanii mmoja anapompuuza mwengine na kuamua kutomjibu mwenzake katika malumbano hususan ya nyimbo na katika mahojiano, hupunguza makali ya mchakato mzima wa bifu na kupunguza utamu. Kutojibiwa kwa msanii Daddy Q na msanii susumila wakati bifu baina yao Mombasani kwatajwa kutompa nafasi Daddy Q kupata umaarufu, huku hatua ya rudeboyz kumjibu susumila kukionekena kama hatua iliyosaidia kupatikana kwa umarufu kwa uhasama baina yao na pia kusambaa kwa jina la msanii susumila.

Je kufikia hapa inatosha kusema kuwa bifu ni jambo jema au baya kwa sanaa ya muziki? Mie nimechokoza mjadala tu, nakuachia wewe msomaji uuendeleze nauamue.


Kwa mengi Zaidi usikose kumskiza Sista Shaniz a.k.a Anti-Virus katika "Show Nambari Moja Mkoani Pwani™" - "Kaya Flavaz®" ndani ya RADIOKAYA 93.1Fm Msa 99.7Mlnd - "Kitovu Cha Umoja Wa Pwani ™.


©mwanamgambo2012